Quantcast
Channel: kifltd » BIASHARA
Viewing all 271 articles
Browse latest View live

EU YASAIDIA BILIONI 20 KUKUZA SEKTA YA KILIMO NCHINI TANZANIA

$
0
0

 

 

IMG_1670

Waziri wa Fedha na Uchumi Mhe Dk. Wiliam Mgimwa

 

Na Frank Mvungi na Eleuteri Mangi-MAELEZO

 

SERIKALI ya Tanzania imetiliana saini mkataba na Jumuiya ya  Umoja wa nchi za Ulaya( EU) utakaowezesha Tanzania kupatiwa shilingi bilioni 20 kusaidia maendeleo katika sekta ya kilimo cha miwa kwa wakulima wa Visiwa vya Zanzibar.

 

 Mkataba huo ulisainiwa jana jijini Dar es salaam kati ya Waziri wa Fedha na Uchumi Mhe Dk. Wiliam Mgimwa na Balozi wa EU Mhe. Filiberto Sebregondi, ambapo unategemewa kuisaidia serikali katika kuondoa umasikini kwa wananchi wake na kuiwezesha nchi kupiga hatua ya maendeleo kupitia sekta ya kilimo.

 

 Waziri Mgimwa alisema kuwa msaada huo pia utasaidia kuwajengea wananchi uwezo  wa kutekeleza kilimo chenye tija na kupanua soko la bidhaa zitokanazo na miwa kwani miundo mbinu ya maeneo ya Uzalishaji pia itaboreshwa katika utekelezaji wa mradi huo.

 

 “Kwa niaba ya Serikali  ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania napenda kuishukuru jumuiya ya  umoja wa nchi za Ulaya kwa juhudi kubwa wanazochukua kusaidia maendeleo ya nchi yetu, asanteni sana,” alisema Waziri Dk.Mgimwa.

 

 Naye balozi wa EU, Mhe. Filberto Sebrigondi alisema wameridhishwa na mikakati ya serikali katika kuwaletea wananchi wake maendeleo ndio maana wanaendelea kuunga mkono juhudi za serikali ili kusaidia wananchi kufikia maendeleo ya kweli hivyo  wameamua kusaidia sekta ya miwa ili iweze kukua na kuchangia katika maendeleo ya Taifa.

 

 Pia balozi Sebrigondi alisema kuwa wataendelea kusaidia bajeti ya Serikali ya Tanzania katika miradi mbalimbali ya maendeleo kwa kuwa Tanzania imeonyesha nia ya dhati katika kukuza uchumi wake na kuweka mazingira mazuri kwa wananchi wake ili waongeze tija katika uzalishaji.

 

 Alisema katika kipindi kilichopita asilimia 87% ya fedha lizizotolewa kwa Serikali ya Tanzania zimeshatumika katika miradi ya maendeleo, hivyo ameahidi  kuwasaidia wanachi wanaojihusisha na kilimo cha miwa ili kuwajengea uwezo, kufanya tafiti na kutoa elimu ya utunzaji mazingira katika maeneo yatakayonufaika na msaada huo.

 

 Umoja wa nchi za Jumuiya ya Ulaya umekuwa kwa muda mrefu ukisaidia sekta mbalimbali za maendeleo hapa nchini ikiwa ni moja ya washirika wa maendeleo  wa Tanzania ambapo baadhi ya Sekta zinazonufaika ni sekta ya kilimo cha Kahawa, na Miwa, sekta ya Barabara, Elimu, nishati ya Umeme ambazo zimesaidia kwa kiasi kikubwa kukuza uchumi wa Tanzania.



BATULI AKIINGIA ‘SHOOTING’ ANAPANDISHA MARUHANI

$
0
0

Na Imelda Mtema
MCHEZA sinema mwenye mvuto wa kipekee Bongo, Yobnesh Yusuf ‘Batuli’ amefunguka kuwa kila aingiapo kwenye kazi ya kurekodi filamu, anapatwa na tatizo la kupandisha maruhani, jambo linalomkosesha raha.
Akizungumza na Exclusive Star, Batuli alisema kuwa hapendi kumhisi vibaya mtu yeyote juu ya tatizo hilo lakini hali hiyo inamkosesha amani kwani haelewi chanzo cha tatizo lake ni nini.
“Mimi kwa kweli sitaki kabisa kuweka imani tofauti ya kumhisi mtu vibaya ila najiuliza kwa nini nipandishe maruhani wakati wa kurekodi peke yake?” alisema Batuli.
Batuli aliongeza kuwa kinachomchosha zaidi hata akienda hospitali, huwa haonekani kama ana tatizo lolote, hali ambayo inampa mawazo zaidi.
 “Namuomba Mungu anisaidie kwa maana hata tatizo lenyewe hospitali halionekani, inanitisha kweli,” alisema Batuli.


Multichoice Tanzania yajikita katika kusambaza Digitali katika shule za msingi Tanzania.

$
0
0

 

 

 

Meneja Uhusiano wa MultiChoice Tanzania, Barbara Kambogi akiwakaribisha wageni wanahabari katika hafla mchapalo ya kusheherekea Africa Day na Dstv ambapo amesema DStv inatoa nafasi kwa wateja wake kuwa na fursa ya kuchagua vifurushi mbalimbali kulingana na uwezo wa mteja ambacho cha uwezo wa chini kabisa ni Access chenye zaidi ya channeli 40 gharama yake ni nafuu sana ambapo mteja atalipia shilingi 16,500 kwa mwezi. (Picha na Zainul Mzige wa dewjiblog).

 

 

 

 

Meneja wa Fedha wa kampuni ya Multichoice Tanzania, Bw. Francis Senguji akizungumzia malengo ya DStv Tanzania ambapo amesema wao kama waendeshaji wa biashara nyingine barani Afrika wanaojali na kuthamini maendeleo ya jamii wameona ni wajibu kusaidia jamii ili kuweza kuendeleza maendeleo ya kijamii nchini Tanzania.

 

 

 

Kwa kuendeleza hilo Multichoice ina mfumo wa kutoa elimu mashuleni ( Multichoice Resource Centre) hivyo watamumia jukwaa la Teknolojia kama darasa kwa njia mbalimbali kuwapa jamii nafasi ya kuendeleza vipaji na ujuzi.

 

 

 

Mfumo huo kutoa rasilimali kwenye shule kama vile ving’amuzi vya Satellite, VCRs/DVD na kifurushi cha elimu cha Dstv. Mpaka sasa Multichoice imeanzisha vituo vya rasilimali jamii katika shule 82 nchi nzima kwenye mikoa ya Arusha, Dar es Salaam, Dodoma, Iringa, Kagera, Mbeya, Pwani na Tanga.

 

 

 

 

Meneja Uendeshaji wa Multichoice Tanzania, Ronald Shelukindo (katikati) akifafanua jambo wakati wa hafla mchapalo katika kusheherekea usiku wa Africa Day na DStv. Kulia ni Meneja Masoko wa Kampuni hiyo Furaha Samalu na kushoto ni Meneja Uhusiano wa Kampuni hiyo Barbara Kambogi.

 

 

 

 

Kutoka kushoto ni Meneja Masoko wa Multichoice Tanzania Furaha Samalu, Blogger John Bukuku wa Fullshangwe Blog, Meneja Uendeshaji wa kampuni hiyo Ronald Shelukindo, Mdau wa DStv na Meneja wa Fedha katika kampuni hiyo Bw. Francis Senguji wakipozi kwa picha.

 

 

 

Kwa taswira zaidi tembelea Mo.blog

TASWIRA KUTOKA IKULU:RAIS JAKAYA KIKWETE AHUDHURIA KIKAO CHA SADC CAPE TOWN

$
0
0

 

  Rais Dk. Jakaya Kikwete akiagana na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Misaada la Marekani USAID, Dk. Rajiv Shah muda mfupi baada ya kufanya naye mazungumzo katika Ukumbi wa Cape Town Convention Center jana
 Rais Kikwete na Mwenyeji wake Rais Jackob Zuma wa Afrika Kusini wakitoka katika ukumbi wa hoteli ya Westin jijini Cape Town Afrika ya Kusini mara baada ya kumalizika kwa kikao maalum cha Kamati ya Ulinzi na Usalma ya SADC kilichofanyika leo. Rais Kikwete alikuwa nchini Afrika Kusini kwa ziara ya kikazi ya siku mbili.
  Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya SADC Rais Kikwete, akijadiliana jambo na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Maendeleo ya Uchumi Kusini Mwa Afrika SADC Dk..Tomaz Salomao jijini Cape Town, Afrika ya Kusini leo wakati wa kikao cha kamati hiyo.
  Rais Kikwete (wa tatu kushoto) akiongoza Kikao Maalum cha Kamati ya Ulinzi na Usalama ya SADC kilichofanyika jijini Cape Town Afrika Kusini leo.Wengine katika picha ni wajumbe wa kamati hiyo akiwemo mwenyeji Rais Jackob Zuma wa Afrika Kusini (kulia), Waziri wa Mambo ya nchi za nje wa Namibia Bibi Netumbo Nandi-Ndaitwa (kushoto), na wa pili kushoto ni Katibu Mkuu wa SADC Dk. Tomaz Salomao.
Rais Dk. Jakaya Kikwete akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji na Mratibu wa Asasi ya Bill and Melinda Gates Foundation, Mark Suzman jijini Cape Town, Afrika ya Kusini. Kulia ni Naibu Waziri wa Kilimo Adam Malima.Picha na Freddy Maro-IKULU

KAMANDA KOVA AKANUSHA TAARIFA ZA KULIPULIWA KWA KANISA LA KKKT KUNDUCHI

$
0
0

 

 

KAMANDAKOVAJeshi la polisi Kanda maalumu ya Dar es salaam  limekanusha taarifa zilizozagaa kuwa kanisa la KKKT Usharika wa  Kunduchi  limelipuliwa na bomu leo hii.Kamanda Suleiman Kova ameiambia radio Uhuru Fm kuwa taarifa hizo hazina ukweli wowote na ni za uzushi kwani jeshi la Polisi lilirusha bomu la machozi wakati likitafuta waharifu waliokuwa jirani na kanisa hilo.


Lady Jay Dee kuripoti Mahakama ya Kinondoni kesho

$
0
0

 

 

 

jd 36b09

Na Andrew Chale
MWANAMUZIKI nguli wa bongo na kiongozi wa yenye mvuto nchini bendi ya ‘Machozi’, Judith Wambura ( Lady JayDee) au Jide ama #Teamaanaconda#, anatarajia kuripoti Mahakama ya Kinondoni siku ya Jumatatu Mei 13, kufuatia kufikishiwa kwa taarifa hizo Gadna G Habash ‘Captain’ ambaye ni Meneja na mume wa Lady Jay Dee. 

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi mchana wa leo, Gadna alisema ni kweli wamepata taarifa za kutaarifiwa kwa Lady Jay Dee kufika Mahakama ya Kinondoni, siku ya Jumatatu.
“Ni kweli tumepata wito na Mahakama ya Kinondoni, Hii ni kufuatia kwa jana kufika watu ambao walijielezea kuwa wanatoka Mahakama hiyo na walikuja na barua ya kumkabidhi Lady Jay Dee mwenyewe hata hivyo hawakumkuta” alisema Gadna.
Aliendelea kueleza kuwa, hata alipowaeleza watu hao wamkabidhi yeye hiyo barua watu hao walisema ilikuwa si lahisi zaidi alitakiwa akabidhiwe mlengwa, hivyo kumueleza kuwa wito wa kufika mahakamani siku ya Jumatatu, na aliwakubalia kwa hilo.
Hata hivyo, Gadna alisema hajajua Lady Jay Dee anaitiwa nini na kwa sababu ya nani zaidi amemwelezea na amesema watatekeleza wito huo wa kufika Jumatatu Mahakamani hapo.
Aidha, kupitia kwenye ukurasa wake wa Kijamii wa facebook, Lady Jay Dee aliandika: “Ratiba ya Usiku wa leo, ni Machozi Band, kama kawaida, ila ratiba ya Jumatatu natakiwa Mahakama ya Kinondoni..Taarifa zaidi zitafuata nikijua kinachoendelea…” aliandika Jide kwenye ukurasa huo ambao mpaka hatua ya mwindishi anatembelea ‘post’ hiyo ilikuwa na maoni mengi ambayo watu mbalimbali walipata kuchangia.
Maoni hayo yanayokaribia zaidi ya 558 na, ‘Like’ zaidi ya 756 na ‘Share’ zaidi ya 20, ambapo wengi wao wameweza kumuhusisha moja kwa moja na Mkurugenzi wa Clouds Fm, Ruge Mutahaba kuwa ndie aliyefanya hivyo.
Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali na moja ya gazeti hivi karibuni ilimnukuu Ruge kuwa amejiandaa kuchukua hatua ikiwemo ya kisheria dhidi ya Lady Jay Dee baada ya kumsema kupitia kwenye mitandao ya kijamii.


9 Attributes Of The Best Entrepreneurial Leaders.

$
0
0

 

 

Creating and building a business is not a one-man show. It requires a team effort, or at least the ability to build trust and confidence among key players, and effectively communicate with partners, team members, investors, vendors, and customers. These actions are the hallmark of an effective leader.

 

Behind the actions are a set of principles and characteristics that entrepreneurial leaders, like Bill Gates and Steve Jobs, seem to have in common. Look for these and nurture them in your own context to improve the odds of success for your own start up:

 

1. Clarity of vision and expectations. You must be able and willing to communicate to everyone your vision, goals, and objectives. Just as importantly, you have to be absolutely clear about who you are, what you stand for, and what you expect from everyone around you. People won’t follow you if they are in the dark or confused.

 

2. Willingness to make decisions. It is often said that making any decision is better than making no decision. Even better than “any decision” is a good decision made quickly. Business decisions always involve risk, at times a great deal of it. Smart entrepreneurs always balance the risk with facts, when they have them, rather than their gut.

 

3. Experience and knowledge in your business area. Effective leaders set a personal standard of competence for every person and function in the start up. It must be clear that you have the knowledge, insight, and skill to make your new company better than your very best competitor.

 

4. Commitment and conviction for the venture. This commitment must be passionate enough to motivate and inspire people to do their best work, and put their heart into the effort. Behind the passion must be a business model that makes sense in today’s world, and a determination to keep going despite setbacks.

 

5. Open to new ideas and creativity. In business, this means spending time and resources on new ideas, as well as encouraging people to find faster, better, cheaper, and easier ways to produce results, beat competition, and improve customer service. Be a role model and guide others to excel.

 

6. Courage to acknowledge and attack constraints. An effective leader is willing and able to allocate resources to remove obstacles to the success of the start up, as well as removing constraints on individuals on the team. It is believing that where there is the will, there will be a way.

 

7. Reward continuous learning. You have to encourage everyone to learn and grow as a normal and natural part of business. That means no punishment for failures, and positive opportunities for training and advancement. Personally, it means upgrading your own skills, listening, and reading about new developments and approaches.

 

8. Self-discipline for consistency and reliability. An effective leader is totally predictable, calm, positive, and confident, even under pressure. People like to follow someone when they don’t have to “walk on eggshells” to avoid angry outbursts, or assume daily changes in direction.

 

9. Accept responsibility for all actions. Everyone and every company makes mistakes. Good entrepreneurs don’t want to be seen as perfect, and they have to be seen as willing to accept the fact that “the buck stops here.” No excuses, or putting the blame on the economy, competitors, or team members.

 

The good news is that all of these principles of leadership are learnable. The bad news is that it’s not easy. Don’t assume that success as an entrepreneur is only about great presentations, killing competitors, or having insanely great ideas. It’s really more about leadership, understanding the needs of your prospective clients, and communicating your solutions with clarity.Source:moeblog


MATOKEO MABOVU YA KIDATO CHA NNE YATACHELEWESHA MATOKEO YA KIDATO CHA SITA

$
0
0

 

 



Matokeo ya mtihani wa kidato cha sita yaliyotarajiwa kutangazwa mwezi  huu yatachelewa  ili kutoa nafasi kwa Baraza la Mitihani la Taifa (Necta),  kurekebisha matokeo mabaya ya mitihani  kidato cha nne ya mwaka jana yaliyofutwa na serikali  mwezi huu.
 
Matokeo ya kidato cha sita ambayo huwa yanatangazwa mwanzoni  mwa mwezi Mei mpaka sasa hayajatolewa  na kwamba hayatatangazwa mpaka matokeo mapya ya kidato cha nne yatakaporekebishwa rasmi.

Alipoulizwa  juu ya suala hilo, Naibu Waziri   wa Elimu na  Mfunzo ya Ufundi  Philipo Mulugo alisema ingawa wakati huu ndio unaopaswa yatangazwe matokeo ya kidato cha sita haitafanyika hivyo hadi yatangazwe matokeo mapya ya kidato cha nne baada ya kufutwa.


Hata hivyo, akasema huenda yakatolewa  pamoja au yakafuata wakati mwingine lakini mara baada ya  kukamilisha kazi ya kurejea na kusahihisha matokeo ya kidato cha nne.


“Siyo kwamba yamechelewa kwani muda wa kujiunga na chuo ni Septemba hivyo haitawaathiri kwa hilo,” alisema Mulugo.


Kuhusu hatma ya wanafunzi wa kidato cha nne ambao wapo mashuleni wanaendelea na masomo ya kidato cha sita, alisema  kama kutakuwa na wanafunzi ambao wapo madarasani  shule zilizowasajili  zitakuwa hazijafuata mfumo wa elimu unavyoelekeza.

Alifafanua kuwa mfumo wa elimu kwa kidato cha nne ulibadilishwa na kwamba endapo mwanafunzi akifaulu anatakiwa kujiunga rasmi kidato cha sita  Julai na si vinginevyo.

Alisema licha ya  ucheleweshaji  wa matokeo  hali hiyo haikuwaathiri wanafunzi hao kwa kuwa ratiba ya kwenda masomoni  haijaanza kwa mujibu wa kalenda  ya shule ya serikali.


Serikali ilifuta matokeo ya kidato cha nne ya 2012 na kuiagiza Necta kuyaandaa upya kwa kutumia utaratibu wa usahihishaji na upangaji madaraja uliotumiwa mwaka  2011

Taarifa ilisema mfumo uliotumika  mwaka jana na kusababisha wanafunzi kushindwa vibaya haukufanyiwa utafiti na maandalizi ya kutosha kabla ya kutumika. 

Matokeo hayo  yaliyotangazwa  mwezi  Februari mwaka huu yalionyesha kuwa asilimia 60 ya wanafunzi walishindwa mtihani.


ALIYEFUMANIWA NA DENTI… FAINI DOLA 400

$
0
0

Issa Mnally na Richard Bukos
YULE mfanyabiashara ‘alwatani’ wa jijini Dar ambaye hivi karibuni alifumaniwa gesti akiwa na mwanafunzi wa kidato cha pili, huenda akapandishwa kizimbani siku yoyote, Ijumaa Wikienda limeinyaka.
Kwa mujibu wa dada wa mwanafunzi huyo ambaye aliomba jina lake lisiandikwe gazetini, baada ya mfanyabiashara huyo kufumaniwa na binti huyo mwenye umri wa miaka 16, aliahidi kutoa fedha za Kimarekani dola 400 (zaidi ya Sh. 640,000) kama faini kwa kitendo hicho.
Hata hivyo, pamoja na kukubali kutoa kiasi hicho, mfanyabishara huyo hakutimiza ahadi yake na kuamua kuingia mitini.
Dada wa mwanafunzi huyo aliliambia Ijumaa Wikienda kwamba mfanyabiashara huyo anasakwa ili wamburuze mahakamani kutokana na mwisho wa mwezi uliopita kushindwa kutimiza ahadi yake.
“Aliandika kwa mkono wake kwamba atamlipa huyu mwanafunzi fedha hizo kama fidia ili akalipie ada ya kuendelea na masomo, lakini mpaka leo hii hajaonekana na wala simu yake ya mkononi haipatikani, tukimkamata tutamburuza mahakamani kwa sababu sheria hapa Bongo hazifuatwi kabisa kwani tulitarajia vyombo husika vingeingilia kati lakini hakuna lolote,” alisema dada huyo.
Aidha, dada huyo alisema kuwa wanatarajia kwenda kuchukua hati ya kumkamata mfanyabiashara huyo ‘RB’ katika Kituo cha Polisi cha Oysterbay, Dar ili waweze kumsaka.
“Ushahidi tunao tena wa uhakika kabisa, kaandika kwenye karatasi na katia saini yake, tena mwandishi naomba na zile picha alizopigwa akiwa chumbani na mdogo wangu ili zinisaidie katika ushahidi wa mahakamani,” alisema dada huyo huku akionesha karatasi ambayo waliingia makubaliano ya kulipwa dola hizo 400 na mfanyabiashara huyo.
Jumatano ya Aprili 24, mwaka huu mfanyabiashara huyo alifumaniwa na denti huyo katika chumba namba 107 ndani ya gesti moja iliyopo Kinondoni, Dar na habari yake kuandikwa kwenye Gazeti la Risasi Jumamosi la Aprili 27.Chanzo:www.globalpublishers.info


MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AKUTANA NA MCHUNGAJI DKT. MATHEW BYAMUNGU NA MKEWE IKULU DAR LEO

$
0
0

 

 

1Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na Mchungaji Dkt. Mathew Byamungu, wakati akimkaribisha Ofisini kwake Ikulu jijini Dar es Salaam, leo Mei 13, 2013 alipofika kwa mazungumzo akiwa ameongozana na mkewe, Je-Ynung. Picha na OMR

 

 

 

2Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Mchungaji Dkt. Mathew Byamungu na mkewe, Bi. Je-Ynung Byamungu, wakati walipofika Ofisini kwa Makamu leo Mei 13, 2013 kwa mazungumzo. Picha na OMR


KIINGILIO MECHI YA SIMBA, YANGA 5,000/-

$
0
0
Kiingilio cha chini kwenye mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya Simba na Yanga itakayochezwa Jumamosi (Mei 18 mwaka huu) kitakuwa sh. 5,000. Kiingilio hicho kwa viti vya rangi ya kijani ambavyo ni 19,648.

Kwa upande wa viti vya rangi ya bluu kiingilio ni sh. 7,000, viti vya rangi ya chungwa itakuwa sh. 10,000, VIP C kiingilio ni sh. 15,000, VIP B itakuwa sh. 20,000 wakati VIP A yenye viti 748 tu tiketi moja itapatikana kwa sh. 30,000. 
Tiketi zitaanza kuuzwa siku moja kabla ya mchezo huo utakaoanza saa 10 kamili jioni.
Mwamuzi wa mechi hiyo atakuwa Martin Saanya kutoka Morogoro ambapo atasaidiwa na Samuel Mpenzu wa Arusha, na Jesse Erasmo kutoka Morogoro. Mwamuzi wa akiba ni Hashim Abdallah wa Dar es Salaam.
Kamishna wa mechi hiyo atakuwa Emmanuel Kavenga kutoka Mbeya wakati mtathmini wa waamuzi (referees assessor) ni Leslie Liunda.
Angetile Osiah
Katibu Mkuu
Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)


GAZETI LA DAR KOMEDI:PREZZO AWACHANGANYA DIVA WA CLOUDS FM NA LADY BOSS

MANYWELE ENTERTAINMENT INAKULETEA KIGOLI WA TZ 2013

Barua kwa Waziri wa Viwanda na Biashara Mh. Dkt. Abdallah Kigoda : Pendezo kuhusu kuzuia Unyonyaji Dhidi ya Wasanii wa Tanzania katika Biashara ya Miito(Ring back tones)

$
0
0

 

 

 

 

 

Kwenda kwa:        DR ABDALLAH KIGODA, Waziri wa Viwanda na Biashara
Kuhusu:             BIASHARA YA MIITO YA SIMU (RINGBACK TONES)
Kumekuwa na malalamiko makubwa sana kuhusu biashara ya mauzo ya nyimbo kama miito kwenye simu. Malalamiko haya yalianzia kwa wasanii wenyewe na baadaye mimi binafsi niliwasilisha hoja zao Bungeni mwaka 2012. Hata hivyo, hadi sasa malalamiko haya bado hayajapatiwa ufumbuzi na hivyo wasanii kuendelea kunyonywa. Tatizo kubwa katika biashara hii ni USIRIna UNYONYAJI kwa wasanii wa Tanzania. Suala la USIRI lipo Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia. Suala la Unyonyaji lipo Wizara ya Viwanda na Biashara.
USIRI
Biashara hii ya “Ring Back Tones” (RBT) hufanywa na Kampuni za simu (Network providers) kwa kununua maudhui kutoka wachuuzi (Content Providers) ambao nao huingia mikataba na Wasanii (Content Creators). Hakuna sheria yoyote au Kanuni hapa nchini inayoongoza biashara hii na hivyo “Network providers” na “Content Providers” kuwa watu pekee wenye taarifa zote za biashara hii. Kampuni za simu hujumuisha mapato ya biashara hii na mapato yake mengine (Not Ringfenced), hawatoi taarifa za manunuzi ya nyimbo (au ‘content’ nyingine yeyote) kwa wadau na hasa wasanii. Wachuuzi (Content Providers) nao hawatoi taarifa za mauzo kwa wasanii na wanatumia uelewa mdogo wa wasanii kuwasainisha mikataba inayowanyonya. Matokeo yake ni kwamba msanii hupata kiasi cha asilimia mbili tu (2.5%) ya mapato ghafi ya kazi yake. Hivi sasa biashara hii inathamani (turnover) ya takribani shilingi 44 bilioni kwa mwaka.
Suluhisho: Serikali kupitia Wizara ya Mawasiliano iandike kanuni (regulations) zitakazolazimisha makampuni ya simu kuweka wazi mapato yatokanayo na biashara ya RBT (Miito ya simu) kila baada ya miezi 4 (disclosure rules). Kanuni hizi zielekeze makampuni kutoa taarifa za mauzo kwa kila kazi (nyimbo/vichekesho etc.)

UNYONYAJI
Kutokana na usiri ulioelezwa hapo juu, wasanii wamekuwa wakinyonywa kimapato. Kwa mfano Msanii hulipwa mapato yatokanayo na ununuzi wa awali wa kazi yake (wimbo) katika mwezi (downloads).
Lakini mapato yatokanayo na “subscriptions” ambapo mlaji hukatwa shilingi 30 kila siku msanii hapati chochote. Hivyo katika mapato ya sh. 1,300 kila mwezi kwa kila mteja kwa kila wimbo, msanii hupata mgawo wake kutoka shilingi 400 tu za ‘downloads’ na ndio maana wasanii wote nchini hupata 2.5% ya shilingi 44 bilioni zinazokusanywa na Kampuni za Simu.
Nchini Marekani biashara ya miito ya simu (RBT) imetafsiriwa kama maonyesho (Public Performances) na hivyo “copyright Association” ya Marekani imeweka kiwango cha chini cha mrahaba (royalty) ambacho msanii hulipwa. Marekani msanii hulipwa asilimia 10 ya patoghafi linalozalishwa na kazi yake kama muito wa simu.

SULUHISHO
Serikali kupitia Wizara ya Viwanda na Biashara iandike kanuni kwamba mauzo ya kazi za wasanii kama miito ya simu inachukuliwa kama ‘performance’ na kwamba Kampuni za simu zitalipa sio chini ya asilimia 12 (12%) ya mapato ghafi, ambapo asimilia 10% itakwenda kwa msanii na asilimia 2% COSOTA kwa ajili ya usimamizi na Ulinzi wa kazi za Wasanii.
HITIMISHO
Kanuni za Uwazi (disclosure rules) katika biashara hii ya ‘Ring Back Tones’ na mgawo wa haki wa mapato (fair and just revenue share) ndio suluhisho endelevu na litakaloleta tija kwa wasanii wa Tanzania na hata Serikali kukusanya mapato stahili. Kanuni (Regulations) zinazopendekezwa zianze kutumika kuanzia tarehe 1/7/2013

Kabwe Z. Zitto, Mb
Kigoma Kaskazini
Dodoma, 13 Mei 2013.


Nchi ya Afrika Kusini yalaani uingiliaji wa Wamagharibi Syria

$
0
0

 

 

 

Bi.Phumla Williams Msemaji wa serikali ya
 Afrika Kusini

 

Serikali ya Afrika Kusini imeitaka jamii ya kimataifa kuheshimu haki ya kujitawala ya Syria, sanjari na kujiepusha na uingiliaji katika masuala ya ndani ya nchi hiyo.

 

 

 

Phumla Williams Msemaji wa serikali ya Afrika Kusini ameongeza kuwa, wenyewe wananchi wa Syria wanapaswa kuutatua mgogoro wa nchi hiyo bila ya uingiliaji wa madola ya kigeni.

 

 

 

Wiki iliyopita, serikali ya Afrika Kusini ililaani vikali hatua ya ndege za utawala wa Kizayuni wa Israel kushambulia ardhi ya Syria na kutahadharisha kuwa, hatua hiyo itazidisha kuvuruga amani na uthabiti katika eneo la Mashariki ya Kati.

 

 

 

Aidha serikali ya Pretoria imetaka ukomeshwe mpango wa baadhi ya nchi za Magharibi na Kiarabu wa kuyapelekea silaha makundi ya kigaidi nchini humo.


Peroni Jazz Sundays at Velisa’s

DIAMOND ATOBOA KWA NINI KIWEMBE!

$
0
0

Na Sifael Paul
KWA mara ya kwanza nyota wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond’ ameacha gumzo London, Uingereza baada ya kueleza sababu za kwa nini ni kiwembe?

Diamond akiwa na Penny.

Akifunguka katika mahojiano maalum wiki iliyopita na Kipindi cha Sporah Show cha runingani alipokuwa kwenye ziara ya kimuziki nchini humo, Diamond alizungumza ishu kibao za kimapenzi hasa juu ya msururu wa wanawake ambao tayari ametoka nao.
ASISITIZA ANASUBIRI MTOTO
Kabla ya yote, staa huyo alisisitiza kuwa muda si mrefu anatarajia kupata mtoto kutoka kwa mpenzi wake wa sasa, Peniel Mungilwa ‘Penny’ akimaanisha kuwa ni mjamzito, kinyume na msichana huyo ambaye hivi karibuni alimshangaa Diamond kueneza habari hizo.

…akiwa na Wema.

KWA NINI ANAPENDA KUBADILISHA WANAWAKE?
Diamond: Mimi ni binadamu kama binadamu wengine wa kawaida. Nampenda mwanamke anayenipenda na kuniheshimu. Ikitokea mikwaruzano huwa mimi nakaa pembeni, natafuta sehemu nyingine. Wakati mwingine mimi ndiye huwa naachwa.
KWA NINI MSURURU NDANI YA KIPINDI CHA MIAKA MITATU?
Diamond: Nikiwa na mtu nikiachana naye naonekana nina matatizo kwa sababu wakati mwingine nakuwa na wanawake wenye majina. Siwezi kukaa bila uhusiano na nakuwa wazi kwa sababu lazima itajulikana tu na kuandikwa kwenye magazeti. Kuna kipindi nilikaa miezi sita bila kufanya kitu chochote (mh!). Lakini nikianza (uhusiano), nikihama naonekana msumbufu.

…akiwa na Jokate.

KWA NINI MASTAA, TENA MARAFIKI?
Diamond: Huwa sitoki, nakuwa nyumbani tu, nakaa na mama yangu (Sanura Kassim ‘Sandra’) nampikia. Nikitoka nakwenda kwenye shoo au studio. Huko ndiko nakutana nao (mastaa wa kike).
ALIMPATAJE JOKATE (MWEGELO)?
Diamond: Alikuwa anazindua nguo zake (Kidoti) akaniomba nikapite nazo kwenye onesho la mavazi, nikapita nazo jukwaani. Baada ya hapo na mimi nilimuomba nifanye naye video ya wimbo wangu (Mawazo), ndiyo ikatokea kama hivyo.
NINI KILIMVUTIA KWA PENNY?
Diamond: Kwanza mimi nilimjua Penny kabla ya Wema (Sepetu), alikuwa mshikaji wangu. Ni mwanamke mzuri, wa kileo, ana akili adabu na heshima. Anampenda mama yangu na familia yangu ‘coz’ na mimi nampenda mama yangu (sifa ambazo kwa mujibu wake Wema alizikosa).
KWA NINI ALIMREKODI WEMA?
Diamond: Kila binadamu anajiona yupo sawa na anaonewa. Sipendi kuongea, nitazungumza vibaya. Mapenzi yanaumiza na mimi naumia pia lakini watu wanadhani mimi ndiye muumizaji. Unamwambia mtu kwa nini una mwanaume mwingine.
Anakuzuga sijui ni pedeshee anampa pesa. Mara unamwona na mwanaume mwingine. Mimi siyo maskini lakini sasa mara unamwona na brazameni mwingine ‘then’ washkaji wanakwambia. Wewe unajifanya kuziba masikio mara unasikia ana mwanaume mwingine. Lakini ikafika wakati nikajikuta naumia sana kwenye mapenzi.

…akiwa na Jokate.

Kama ukisikiliza ule wimbo wa Kesho ni kweli kabisa. Mimi nikakaa pembeni hadi nilipompata huyu wa sasa (Penny).
Nakumbuka (Wema) alinipigia simu akadai mimi ndiye nasema anataka turudiane. Nilikuwa kwenye gari, nikamuuliza anataka nini?
Wakati huo nilishafika nyumbani kwa baby wangu. Nikamwonesha ona sasa, anasema mimi ndiyo nataka nirudiane naye, anatangazia watu hadi saluni kuwa nataka kurudiana naye na kujidai kwenye vyombo vya habari kuwa ananipenda. Kumbe ana wengine (ving’asti) kama ishirini anawahonga (mistari ya wimbo wake wa Nataka Kulewa).
Nilimpa baby wangu akamwambia kistaarabu tuache tulale. Sasa kuna mtu wetu wa karibu ndiye aliyehusika kusambaza ile sauti.
SEMA UKWELI, ULILALA NA UWOYA?
Diamond: (kicheko) Ningeanzia wapi? Unajua mimi ni simba kwa hiyo nikionekana na swala inajulikana lazima nimle hata kama tumeenda sehemu tu kuzungumza ishu za kazi.
KWA NINI WANAWAKE AU ENZI ZILE HAKUWA NA ‘CHANSI’ SASA AMEPATA?
Diamond: Ukimuelimisha mwanamke mmoja umeelimisha ulimwengu mzima. Nawapenda sana, wanajaa tele kwenye shoo zangu. Kilichotokea kwa Wema ilibidi tu sikuwa na jinsi.
ANATAKA MWANAMKE WA AINA GANI?
Diamond: Ukimuuliza mwanamke aliyewahi kuwa na mimi atakwambia najua mapenzi, najua kupetipeti, najua kubembeleza, najua kujifanya mjinga. Narudia tena, awe mzuri, wa kileo, mwenye akili, anayejiheshimu, ampende mama yangu kama mimi ninavyompenda mama yangu.

Nasibu Abdul ‘Diamond’.

KWA NINI KIWEMBE?
Uchunguzi uliofanywa na Ijumaa ulibaini kuwa chanzo cha staa huyo aliyetokea Tandale, Dar kuitwa kiwembe ni kutokana na tabia yake ya kubadilisha wanawake kama nguo.
Baadhi ya aliowahi kuripotiwa akidaiwa kutoka nao ni Rehema Fabian (Miss Kiswahili 2009), Jacqueline Wolper (msanii wa filamu), Upendo Moshi ‘Pendo’ (Mshiriki wa Maisha Plus) na  Natasha (Video Queen wa Bongo Fleva).
Wengine ni Wema (mwigizaji), Jokate (mwigizaji), Aunt Ezekiel (mwigizaji), Najma (msanii wa Bongo Fleva), Penny (mtangazaji DTV), Irene Uwoya (mwigizaji) na wengineo.Chanzo:www.globalpublishers.info


President Barack Obama to Visit S’Africa, Tanzania, Rwanda, Considers Stopover in Nigeria

$
0
0
 President Barack Obama of the United States
By Paul Ohia
 
President Barack Obama of the United States is billed to begin his second tour of Africa at the end of June with visits to South Africa, Tanzania and Rwanda.
He will however make a stopover in Nigeria, during which he will hold bilateral discussions with President Goodluck Jonathan and other top government officials.
The initial plan for the African tour was for Obama to spend two days in Nigeria, but owing to insecurity occasioned by the terrorist activities of the Islamic militant group, Boko Haram, the plan was reviewed and he is now expected to spend a few hours or one day in the country.
Sources from the presidency added that security situation during Obama’s visit would be paramount and if there is any reason to doubt Nigeria’s unpreparedness to host the US president, his visit to the country might be cancelled outright.
Obama’s maiden visit to Africa took him to Ghana in July 2009 during which he met with President John Atta Mills, now deceased, and delivered a speech at the Ghanaian parliament in addition to touring a former departing point of the trans-Atlantic slave trade, the Cape Coast Castle.
The non-inclusion of Nigeria on his itinerary in 2009 was widely regarded as a snub and a subtle criticism of the country’s leadership, a perception, which the then Secretary of State, Mrs. Hillary Clinton, dismissed.
She had said Obama’s choice of Ghana was “meant to tea-up” US relationship with sub-Saharan Africa, and the choice should not be interpreted in any other way.
During his visit, the two nations are expected to discuss issues centred on trade relations, security and human rights.For More Info Click Here

MWANANCHI: MWAKYEMBE, SERUKAMBA WAVUTANA

UTEUZI:Rais Jakaya Kikwete Ameteua Mabalozi Kujaza Nafasi Zilizo Wazi Nchini Marekani na Umoja Wa Falme za Kiarabu

Viewing all 271 articles
Browse latest View live